Wednesday 5 May 2010

Bayern kwenda kwa Pilato kwa ajili ya Ribery
Bayern Munich imesema itakata rufaa kwenye Mahakama ya Usuluhishi katika Michezo, CAS [Court for Arbitration for Sports] baada ya UEFA kuitupilia mbali rufaa yao kupinga kufungiwa kwa Mchezaji wao Franck Ribery mechi 3 ikimaanisha ataikosa Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI ambayo Bayern Munich watakutana na Inter Milan Uwanjani Santiago Bernabeau Mei 22.
Ribery alipewa Kadi Nyekundu kwenye mechi ya Bayern v Lyon ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI alipomtimba Straika wa Lyon Lisandro na UEFA ikamwongezea adhabu ya kifungo cha mechi 3.

No comments:

Powered By Blogger