Sunday 2 May 2010

Ubingwa hadi Jumapili ijayo!!!!
Sunderland 0 Man United 1
Manchester United leo wamehakikisha vita vya Ubingwa kati yao na Chelsea vinaendelea hadi Jumapili ijayo wakati mechi za mwisho kabisa za Ligi Kuu zitapochezwa baada ya kuifunga Sunderland huko Stadium of Light kwa bao 1-0.
Kabla ya mechi hii ya Man United, hivi leo Chelsea waliwafunga Liverpool 2-0 na hivyo kuwa mbele ya Man United kwa pointi 4 na kama wangefungwa na Sunderland, leo hii Chelsea angekuwa Bingwa.
Bao la ushindi la Man United lilifungwa na Nani kwenye dakika ya 28.
Mechi za mwisho, Chelsea na Man United wote watachezea Viwanja vya nyumbani kwa Chelsea kuikaribisha Wigan Timu ambayo iliitandika Chelsea bao 3-1 katika mechi ya kwanza ya Ligi na Man United kuwakaribisha Old Trafford vibonde wa Chelsea, Stoke City, waliokung’utwa goli 7-0 na Chelsea.
Ili kuwa Bingwa, Chelsea anahitaji kuifunga Wigan na akishindwa kufanya hilo na Man United wakaifunga Stoke City, Ubingwa utabaki Old Trafford.

No comments:

Powered By Blogger