Monday 3 May 2010

Hull City rasmi wameshuka Daraja!!!
Wigan 2 Hull City 2
Sare ya 2-2 na Wigan katika mechi ya Ligi Kuu ya leo imehitimisha rasmi kushuka Daraja kwa Hull City na kuungana na Timu nyingine mbili, Portsmouth na Burnsley, kwenda kucheza Ligi ya Coca Cola Championship Msimu ujao.
Kwa sare ya leo, Hull City wamefikisha pointi 29 na Timu iliyo juu yao, West Ham, ina pointi 34 na mechi imebaki moja tu hivyo hawawezi kuwafikia West Ham.
Hull City waliongoza 2-1 hadi dakika za majeruhi na hivyo walikuwa wana uwezo, kimahesabu, kurefusha kutoshuka Daraja hadi mechi ya mwisho lakini bao la lala salama la Steve Gohouri wa Wigan la kusawazisha ndio liliwamaliza Hull City.
Katika mechi hii, Wigan walitangulia kupata bao kupitia Moses kwenye dakika ya 30 lakini Hull wakasawzisha dakika ya 42 kupitia Atkinson na Cullen akawafungia bao la pili dakika ya 64.
Ndipo kwenye dakika ya 93 Gohouri alipowakata maini Hull City kwa kusawazisha na kuwaporomosha chini.

No comments:

Powered By Blogger