Thursday 6 May 2010

Mkataba wa Rooney kujadiliwa baadae
Manchester United na Wawakilishi wa Wayne Rooney wamekubaliana kufanya mazungumzo ya kuuboresha Mkataba wa Mchezaji huyo baada ya kumalizika Fainali za Kombe la Dunia.
Mkataba wa sasa wa Rooney bado una miaka miwili kumalizika na unampa Mshahara wa Pauni Elfu 90 kwa wiki na huo mpya unategemewa kumpatia Pauni 150,000 kwa wiki na kumfanya awe na Mshahara wa juu kupita Wachezaji wengine hapo Man United.
Kwa sasa Rio Ferdinand, anaepata Pauni 110,000 kwa wiki, ndie anaelipwa juu zaidi.
Marseille watwaa Ubingwa Ufaransa
Marseille waliwafunga Rennes bao 3-1 na kutwaa Ubingwa wa Ufaransa na hii ni mara ya kwanza kuwa Bingwa tangu mwaka 1992.
Huku Ligue 1 ikiwa imabekisha mechi mbili kumalizika, Marseille wako pointi 8 mbele na hakuna Timu inayoweza kuwakamata.
Marseille ina Wachezaji wengi kutoka Afrika wakiwemo Mamadou Niang kutoka Senegal, Taye Taiwo kutoka Nigeria, Souleymane Diawara toka Senegal, Charles Kabore wa Burkina Faso , Stephane Mbia wa Cameroun na Bakari Kone wa Ivory Coast.

No comments:

Powered By Blogger