Sunday 2 May 2010

Fergie aizungumza Liverpool!!
Mara baada ya Liverpool kupigwa 2-0 kwao Anfield na Chelsea na hivyo kufuta matumaini ya Manchester United ya kutaka Chelsea watibuliwe, Sir Alex Ferguson alipohojiwa alisema: “Si kitu tulichokitaka-hiyo ni kweli! Nilidhani Liverpool wanaweza kufanya kitu. Lakini ni ngumu kutegemea wangewafunga Chelsea. Goli la kwanza? Inaweza kutokea na nina hakika Gerrard atajuta, lakini imetokea. Sisi inabidi tutimize wajibu wetu- na hilo ndio fahari na historia ya Klabu hii!! Hatuwezi kushinda kila kitu. Lakini tukiifunga Sunderland leo, kinyang’anyiro kitaenda hadi siku ya mwisho! Huo ndio ukweli.”

No comments:

Powered By Blogger