Wednesday 5 May 2010

LEO NI FAINALI NAFASI YA 4!!!
Leo saa 4 usiku, saa za bongo, Uwanja wa City of Manchester utazikutanisha Timu za Manchester City na Tottenham Hotspurs zinazogombea ile nafasi lulu, nafasi ya 4 kwenye Msimamo wa Ligi Kuu, ili kuungana na Timu 3 za juu, Chelsea, Manchester United na Arsenal, kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Hadi sasa nafasi hiyo ya 4 imekaliwa na Tottenham wenye pointi 67 na Man City wako nafasi ya 5 wakiwa na pointi 66 na Timu zote hizi zimecheza mechi 36 na wakikutana leo watabakisha mechi moja.
Tottenham wakishinda leo watajihakikishia nafasi hiyo ya 4 lakini wakishinda Man City itabidi Timu hizo zisubiri hadi mechi za mwisho Jumapili ili ipatikane Timu ya 4.
Tottenham wana rekodi nzuri kwa Man City kwani katika mechi ya kwanza ya Ligi waliifunga City bao 3-0.
Msimu uliokwisha Tottenham walishinda mechi zote mbili za Ligi kwa bao 2-1 kila mechi.
Katika mechi ya leo kila Timu itamkosa Kipa nambari wani ambao wameumia na Man City watamchezesha Kipa wa ‘kuazima’ kutoka Sunderland, Martin Fulop.
Kipa wa Tottenham anategemewa kuwa Ben Alnwick kufuatia kuumia kwa Kipa Mbrazil Heurelho Gomes.
Vikosi vinategemewa kuwa:
Manchester City (Fomesheni 4-4-2): Fulop; Zabaleta, Toure, Kompany, Bridge; A Johnson, De Jong, Vieira, Bellamy; Adebayor, Tévez.
Tottenham Hotspur (Fomesheni 4-4-1-1): Gomes; Kaboul, Dawson, King, Assou-Ekotto; Bentley, Huddlestone, Bale; Modric; Crouch.
Refa: Steve Bennett

No comments:

Powered By Blogger