Sunday 2 May 2010

Liverpool 0 Chelsea 2
-Zawadi toka kwa Gerrard yawasogezea Ze Bluzi Ubingwa!!!!!!
Chelsea leo wamejisafishia njia ya kuuchukua Ubingwa walipoifunga Liverpool bao 2-0 huko Anfield na hivyo kujikita kileleni wakiwa pointi 4 mbele ya Manchester United ambao watacheza na Sunderland muda si mrefu.
Chelsea wamebakisha mechi moja watakayocheza kwao Stamford Bridge Jumapili ijayo na Wigan Timu ambayo iliitwanga Chelsea bao 3-1 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu na ushindi dhidi ya Wigan utawapa Chelsea Ubingwa bila ya kujali Manchester United watapata matokeo gani katika mechi zao.
Bao la kwanza kwa Chelsea hivi leo lilikuwa zawadi nono toka kwa Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, ambae alirudisha pasi nyuma kizembe, au makusudi ikiwa ni Man United na unaamini mechi hii ni njama, na kumpasia Dider Drogba aliefunga kilaini dakika ya 33.
Bao la pili lilipachikwa Na Frank Lampard kwenye dakika ya 54.
Fulham 3 West Ham 2
Katika mechi nyingine ya Ligi Kuu Fulham imeipiga West Ham kwa bao 3-2 na mabao ya Fulham yalifungwa na Clint Dempsey, Carlton Cole [kajifunga mwenyewe] na Stefano Okaka.
Mabao ya West Ham yalipachikwa na Carlton Cole na Guillermo Franco.

No comments:

Powered By Blogger