Thursday 6 May 2010

LIGI KUU waigomea Fulham kupanga upya mechi na Ze Gunners
Wasimamizi wa Ligi Kuu England wamelikataa ombi la Fulham la kutaka mechi yao ya mwisho na Arsenal itakayochezwa Jumapili isogezwe mbele na kuchezwa Jumamosi ili wapate muda mrefu zaidi wa kujitayarisha kwa ajili ya Fainali ya EUROPA LIGI ambayo watacheza Jumatano ijayo na Atletico Madrid huko Hamburg, Ujerumani.
Ligi Kuu imelitupa ombi hilo kwa kusema kuwa kwa vile Jumapili ni siku ya mwisho ya Ligi mechi zote zimepangwa kuanza muda mmoja na haitakuwa vyema mechi ya Arsenal v Fulham itakayochezwa Uwanja wa Emirates isogezwe.
Redknapp: “Ni sahihi sisi kucheza UEFA!”
Meneja wa Tottenham, Harry Redknapp, anaamini Timu yake inastahili kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao baada ya kuinyakua nafasi ya 4 walipoifunga Manchester City bao 1-0 hapo jana Uwanjani City of Manchester kwa bao la dakika ya 82 la Peter Crouch.
Redknapp ametamka: “Ulikuwa usiku mwema! Tumecheza vizuri na tulistahili kushinda!”
Tottenham wanamalizia ligi Jumapili kwa kucheza na Burnley na upo uwezekano wa kushika nafasi ya 3 ikiwa watashinda na Arsenal, ambao wako nafasi hiyo, wafungwe na Fulham.

No comments:

Powered By Blogger