Wednesday 5 May 2010

Fergie: Sijuti wala sikasiriki!
Sir Alex Ferguson ametamka hawezi kukaa chini ajute au kukasirika wapi Manchester United walifanya kosa na pengine kuwapa Ubingwa Chelsea Jumapili ijayo.
Jumapili Ligi Kuu inamalizika kwa Chelsea kucheza na Wigan na Manchester United kuikwaa Stoke City.
Ikiwa Chelsea wataifunga Wigan wao ni Mabingwa lakini wakishindwa hilo na Man United wakiifunga Stoke basi Man United watautetea Ubingwa wao.
Ferguson amesema: “Nilikuwa nautazama tena kila mchezo lakini huko ni kujitesa tu! Msimu ulipoanza tulifungwa na Biurnley tukakosa penalti mechi hiyo na hizo ni pointi 3 tumepoteza! Mechi zote na Chelsea Marefa waliwabeba!”
Ferguson amedokeza atafanya mabadiliko kwa ajili ya Msimu ujao na tayari ameshawachukua Wachezaji chipukizi Chris Smalling toka Fulham na Javier Hernandez  toka Mexico.

No comments:

Powered By Blogger