Saturday 1 May 2010

LIGI KUU: Matokeo mechi za Leo
Birmingham 2 v Burnley 1
Man City 3 v Aston Villa 1
Portsmouth 3 v Wolves 1
Stoke 0 v Everton 0
Tottenham 1 v Bolton 0
Vita ya Nafasi ya 4
Tottenham imezidi kujichimbia nafasi ya 4 ya Ligi Kuu na hivyo kuweza kucheza Ulaya Msimu ujao baada ya kuwafunga Bolton bao 1-0, bao lililofungwa na Kiungo Tom Huddlestone Uwanjani White Hart Lane.
Huko City of Manchester Stadium, Man City walitanguliwa bao moja la John Carew wa Aston Villa dakika ya 16 na Carlos Tevez akasawazisha kwa penalti dakika ya 41 na dakika mbili baadae Adebayor akaipatia City bao la kuongoza.
Craig Bellamy alihakikishia ushindi Man City alipofunga dakika ya 89.
Ushindi huu wa Tottenham na ushindi wa Manchester City unaifanya mechi ya Jumatano Uwanjani City of Manchester kati ya Man City na Tottenham iwe kama Fainali ya kuamua nani Bingwa wa nafasi ya 4.
Ukweli ni kuwa Liverpool wana nafasi finyu na Aston Villa tayari washabwagwa kwenye kugombea nafasi ya 4 kwa vile wamebakisha mechi moja tu na hata wakishinda mechi hiyo watafikisha pointi 67 ambazo tayari Tottenham anazo na tatizo nyingine kwa Villa ni kuwa wana tofauti ya magoli machache mno ukilinganisha na Tottenham.
Msimamo kwa wagombea nafasi ya 4 baada ya mechi za leo:
-Tottenham mechi 36 pointi 67
-Man City mechi 36 pointi 66
-Aston Villa mechi 37 pointi 64
-Liverpool mechi 36 pointi 62
Birmingham 2-1 Burnley
Katika mechi ya Ligi Kuu iliyoanza mapema leo, Birmingham walitawala na kuifunga Burnley, Timu ambayo tayari imeshaporomoshwa kwenda kucheza Daraja la chini Msimu ujao, kwa bao 2-1 Uwanjani Mtakatifu Andrew.
Mabao ya Birmingham yalifungwa na Cameron Jerome na Christian Benitez.
Bao la Burnley lilifungwa na Steven Thompson.

No comments:

Powered By Blogger