Thursday 29 April 2010

Man City yapata Kipa
Uhaba wa Kipa ulioikumba Manchester City sasa umekwisha baada ya kumsajili kwa dharura Kipa wa Akiba kutoka Sunderland, Marton Fulop, ili awadakie mechi 3 za Ligi Kuu zilizobaki.
Man City walikumbwa na upungufu huo baada ya Makipa wao wote kuumia na hao ni Kipa Nambari Wani Shay Givens, alieumia kwenye droo ya 0-0 na Arsenal wikiendi iliyopita, Stuart Taylor na David Gonzalez.
Kipa mwingine wao wa kutumainiwa, Joe Hart, yupo Birmingham kwa mkopo na mkataba wake umemzuia kurudi Klabuni kwake Man City hadi Msimu huu unapokwisha.
Furlop alizungumza: “Nilipata simu Jumanne. Na nilifurahi kuja kuisaidia Man City. Itanipa chansi kucheza!”
Nae Meneja wa Sunderland, Steve Bruce, amesema ni nafasi nzuri kwa Kipa wao huyo wa Akiba kucheza kwani Klabuni hapo Kipa Nambari wani ni Craig Gordon, ambae ni Kipa wa Taifa wa Scotland, na ndie amemfanya Furlop kukosa namba.

No comments:

Powered By Blogger