Monday 26 April 2010

Deco kung’atuka Chelsea
Mchezaji wa Kimataifa wa Ureno mwenye asili ya Brazil, Deco, miaka 32, ameamua kuondoka Chelsea Msimu huu ukiisha na kurudi kwao Brazil ili kuendesha Shule aliyoianzisha Nchini humo.
Deco alijiunga na Chelsea mwaka 2008 akitokea Barcelona.
Deco alizaliwa Mji wa Sao Bernardo do Campo huko Brazil na kuhamia Ureno akiwa na miaka 19 na akapata uraia wa Ureno mwaka 2002.
Hata hivyo mwenyewe Deco hajasema kama akiwa huko Brazil ataendelea kucheza mpira au la.
Deco amesema: “Nina rafiki yangu huko Brazil ambae ni Daktari na huniambia ipo siku nitakuwa Mchezaji mpira wa zamani lakini yeye hawezi kuwa Daktari wa zamani! Kuna taaluma nyingi huwezi kuziacha lakini soka lazima unaiacha!”

No comments:

Powered By Blogger