Nusu Fainali: Leo Lyon v Bayern, kesho Barca v Inter

Kesho ndio kindumbwendumbwe huko Nou Camp wakati Wenyeji Barcelona watawania kuifunga Inter Milan kwa bao 2-0 ili waipiku Inter kwa goli la ugenini baada ya kufungwa mechi ya kwanza 3-1 huko San Siro.
Kocha wa Lyon, Claude Puel, amedai wao hucheza vizuri zaidi wakitaka ushindi kuliko wanapokuwa wanajilinda tu na hilo limeungwa mkono na Mfungaji wao mkuu kutoka Argentina, Lisandro Lopez, ambae ametaka mashambulizi mfululizo.
Katika mechi hiyo ya leo Bayern watamkosa Nyota Franck Ribery na Lyon hawatakuwa na Jeremy Toulalan baada ya Wachezaji hao kutolewa kwa Kadi Nyekundu katika mechi ya kwanza.
Vile vile, Bayern huenda wakawakosa Masentahafu wao, Daniel van Buyten na Martin Demichelis, ambao wameumia.
No comments:
Post a Comment