Thursday 29 April 2010

"MTU SPESHELI”: Misifa Mourinho achekelea, asifiwa!!
Kocha mpenda sifa, mwenye kauli za kejeli na machachari, aliebatizwa “Mtu Spesheli”, Jose Mourinho, ameisifia Timu yake Inter Milan kwa kuibwaga Barcelona waliokuwa Mabingwa Watetezi wa Ulaya na wao kuingia Fainali na watakutana na Bayern Munich hapo Mei 22 kupata Bingwa mpya wa Ulaya.
Ingawa Barca walishinda 1-0 hapo jana wametupwa nje kwa jumla ya bao 3-2 baada ya kufungwa mechi ya kwanza 3-1.
Inter walicheza mechi ya jana kwa zaidi ya saa moja huku wakiwa Mtu mmoja pungufu Mchezaji wao Thiago Motta alipopewa Kadi Nyekundu.
Mourinho alinena: “Hii ni bora kuliko kushinda CHAMPIONS LIGI! Barca walitegemea kushinda! Huwa na maajabu Nou Camp lakini tuligundua wanatuogopa!”
Huku akiwa na furaha Mourinho ameihakikishia Inter kuwa atabaki nao Msimu ujao licha ya kuwa na tetesi nyingi kuwa yuko njiani kuondoka.
Mwenyewe alisema: “Naiheshimu Soka ya Italia lakini sina mapenzi na Soka ya Italia! Ntabaki Msimu ujao!”
Kuhusu Refa, Mourinho alizungumza: “Sitaki kumhukumu. Nilisema kabla ya mchezo kama Wachezaji watamsaidia Refa mechi ni nzuri lakini wakiwa wakorofi, kuna matatizo. Na usiku huu, Wachezaji walijaribu kuleta utata na ugumu!”
Nae Rais wa Inter Milan, Massimo Moratti, alimsifia Mourinho na kumwita Bora.
Moratti alisema: “Mourinho ni shujaa! Sasa tupo Fainali 3! Tupo Ulaya, tupo Coppa Italia na kwenye Serie A tuko karibu! Shukrani zote kwa Mourinho! Ni Meneja bora yeye!!”

No comments:

Powered By Blogger