Wednesday 28 April 2010

LISTI YA UBORA FIFA: Brazil Nambari Wani, Spain mbili, England 8 na Bongo yapanda nafasi moja……..ni wa 108!!!!
Brazil wameipiku Spain na kuchukua uongozi na kuwa Timu Bora Duniani kwa mara ya kwanza baada ya Miezi mitano kufuatana na Listi ya FIFA.
Spain wako nafasi ya pili.
Ureno imepanda hadi nafasi ya 3 na hii ikiwa nafasi ya juu kwa wao kuifikia.
Argentina wamepanda nafasi mbili na kushika nafasi ya 7 na hivyo England kushuka hadi nafasi ya 8.
Holland wako nafasi ya 4, Italy ya 5, Ujerumani ya 6 na Croatia nafasi ya 9.
Timu kutoka Afrika ambayo iko nafasi ya juu kabisa ni Misri iliyo nafasi ya 13 baada ya kupanda nafasi moja.
Katika Nchi za afrika ambazo ziko Fainali ya Kombe la Dunia, Cameroun ndio wako juu na wapo nafasi ya 19 baada ya kupanda nafasi moja.
Tanzania nayo imepanda nafasi moja na kushika namba ya 108.

No comments:

Powered By Blogger