Thursday 29 April 2010

Leo ni Marudiano NUSU FAINALI: Liverpool v Atletico Madrid na Fulham v Hamburg
Liverpool leo wako kwao Anfield wakitaka kuupinndua ushindi wa bao 1-0 wa Atletico Madrid katika mechi ya kwanza ili wasonge na kuingia Fainali ya EUROPA LIGI.
Nako huko Craven Cottage kwenye marudio ya Nusu Fainali nyingine, wenzao Fulham watawakaribisha Hamburg waliotoka nao sare 0-0 kwenye mechi ya kwanza huko Ujerumani.
Timu zote, Liverpool na Fulham, zilipata taabu mno kwenda kucheza mechi zao za kwanza za ugenini za huko Spain na Ujerumani pale walipolazimika kutumia usafiri wa ardhini wa Treni, Meli na Mabasi kwa vile wiki iliyopita Ulaya ilikumbwa na balaa la Majivu ya Volcano kutoka Iceland iliyosababisha safari za anga kusimama.
Balaa hilo leo halipo na Atletico Madrid na Hamburg zimesafiri raha mustarehe kwenda kwnye vituo vyao vya Miji ya London na Liverpool kwa ndege.

Inter Fainali!!!! Barca washinda lakini njeee!!!!
Barcelona, mbele ya Mashabiki wao 98,000, walishindwa kuingia Fainali itayochezwa kwenye Uwanja wa Mahasimu zao wakubwa Real Madrid, Uwanja wa Santiago Bernabeau hapo Mei 22, licha ya kuifunga Inter Milan bao 1-0 na hivyo kutolewa nje kwa jumla ya mabao 3-2 kwa vile Inter Milan walishinda mechi ya kwanza 3-1.
Inter Milan walijihami vizuri mno licha ya kucheza Mtu 10 kwa zaidi ya saa moja baada ya Thiago Motta kutolewa kwa Kadi Nyekundu na Refa kutoka Ubelgiji Frank de Bleeckere kwa kumpiga Sergio Busquets.
Bao lililowapa matumaini Barca lilifungwa na Gerrard Pique dakika 6 kabla mpira kwisha na Barca walifunga tena dakika za majeruhi kwa bao la Bojan lakini Refa alilikataa kwa kufanyika madhambi kabla ya kufungwa.
Inter Milan watakutana na Bayern Munich kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI na hii ni Fainali ya kwanza ya Ulaya kwa Inter tangu 1972.

No comments:

Powered By Blogger