Saturday 1 May 2010

LIGI KUU WIKIENDI: Bigi Mechi ni Jumapili Liverpool v Chelsea!!!!
Ingawa leo Jumamosi kuna mechi kadhaa na muhimu kwa Timu zinazogombea nafasi ile ya 4 ili wacheze Ulaya Msimu ujao, macho na masikio yetu sote yapo Jumapili hasa kwa ile BIGI MECHI kati ya Liverpool na Chelsea huko Anfield na itafuatiwa na Sunderland v Manchester United huko Stadium of Light.
Huku zikiwa zimebaki mechi mbili Ligi kwisha, Chelsea yupo kileleni kwa pointi moja dhidi ya Man United.
Ikiwa Chelsea atateleza kwa Liverpool kwa ama kutoka sare au kufungwa na Man United kumfunga Sunderland, uongozi utatwaliwa na Man United na Timu zote zitabakiza mechi moja tu.
Liverpool bado ana nafasi finyu ya kuipata nafasi ya 4 na hivyo kucheza Ulaya Msimu ujao.
Arsenal wao tayari wamefuzu kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI na Ubingwa washawapisha Chelsea na Man United kuugombea.
Nafasi ya 4 bado inagombewa na Tottenham, Man City, Aston Villa na Liverpool.
Everton wao wapo kwenye vita ya kuipata nafasi ya 7 ili wacheze EUROPA LIGI Msimu ujao.
Huko mkiani tayari Timu mbili kati ya 3 zinazoporomoka Daraja zishapatikana na nazo ni Portsmouth na Burnley.
Timu ya mwisho kuungana na Portsmouth na Burnley, bila shaka, ni Hull City ambao wako pointi 6 nyuma ya West Ham na ndio wenye nafasi kubwa ya kuungana na Portsmouth na Burnley labda washinde mechi zao mbili zilizobaki na West Ham wafungwe mbili zao zilizobaki na tofauti ya magoli iliyopo kati yao ya goli 23 ifutwe katika matokeo ya mechi hizo mbili zilizobaki.
RATIBA:
Jumamosi, 1 Mei 2010
[saa 8 dak 45 mchana]
Birmingham v Burnley
[saa 11 jioni]
Man City v Aston Villa
Portsmouth v Wolves
Stoke v Everton
Tottenham v Bolton
Jumapili, Mei 2
[saa 9 na nusu mchana]
Liverpool v Chelsea
[saa 11 jioni]
Fulham v West Ham
[saa 12 jioni]
Sunderland v Man United
Jumatatu, Mei 3
[saa 9 na nusu mchana]
Wigan v Hull
[saa 1 usiku]
Blackburn v Arsenal
MSIMAMO LIGI KUU England:
[KILA TIMU IMECHEZA MECHI 36 ISIPOKUWA INAPOTAJWA]
1. Chelsea pointi 80====KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
2. Man United 79======KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
3. Arsenal 72========KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
4. Tottenham mechi 35 pointi 64
-------------------------------------------
5. Aston Villa 64
6. Man City mechi 35 pointi 63
7. Liverpool 62
8. Everton 57
9. Birmingham 47
10. Sunderland 44
11. Blackburn 44
12. Fulham mechi 35 pointi 43
13. Stoke mechi 35 pointi 43
14. Bolton 36
15. Wolves 35
16. Wigan 35
17. West Ham 34
--------------------------------------
18. Hull City 28
19. Burnley 27==========IMESHUSHWA
20. Portsmouth 16=======IMESHUSHWA
--------------------------------------------------------------
MECHI SPESHELI za Jumamosi:
Man City v Aston Villa
Hii ni vita ya kugombea ile lulu ya nafasi ya 4 ili kucheza Ulaya Msimu ujao na vita hii ipo ndani ya City of Manchester Stadium.
Nafasi hiyo ya 4 imeshikwa na Tottenham waliocheza mechi 35 na wana pointi 64 sawa na Aston Villa waliocheza mechi moja zaidi.
Man City wao wamecheza mechi 35 na wana pointi 63.
Villa hawajafungwa katika mechi 5 zilizopita na wameshinda 3 kati ya hizo na Man City walitoka sare na Arsenal ya 0-0 wikiendi iliyopita.
Baada ya mechi hii, City watacheza na Tottenham Jumatano katika vita nyingine ya nafasi ya 4.
Man City, waliopata hofu ya kukosa Kipa baada ya Makipa wao wote kuumia, tayari washamchukua kwa mkopo wa dharura Kipa wa Akiba wa Sunderland, Martin Fulop, ili awadakie mechi zao tatu zilizobaki.
Tottenham v Bolton
Tottenham, wanaokalia Taji linalotafutwa kwa udi na uvumba la nafasi ya 4 kwenye Ligi, wapo nyumbani White Hart Lane kuwakaribisha Bolton Wanderers.
Baada ya kuzichapa mfululizo Chelsea na Arsenal, Tottenham walikung’utwa mechi yao iliyofuatia wikiendi iliyokwisha na Mabingwa Watetezi Manchester United kwa bao 3-1 huko Old Trafford na leo watataka kufuta machungu hayo na kujikita nafasi ya 4 kwa kuifunga Timu inayoelea kwenye bahari ya Ligi Kuu, Bolton, bila misukosuko ya kushuka Daraja au kucheza Ulaya.

No comments:

Powered By Blogger