Monday 26 April 2010

Man City hawana Kipa!!!
Manchester City wamepeleka ombi la dharura kwa Wasimamizi wa Ligi Kuu ili waruhusiwe kusajili Kipa kwa mkopo wa dharura ili waweze kumaliza mechi zao 3 za Ligi Kuu zilizobaki na kuweza kufanikisha azma yao kuinyaka nafasi ya 4 kwenye Ligi na hivyo kucheza Ulaya Msimu ujao.
Ghafla majeruhi kwa Makipa wao imeifanya Man City ikose Kipa wa kutegemewa hata mmoja.
Kipa wao nambari moja Shay Givens aliteguka bega Jumamosi Uwanjani Emirates walipotoka droo na Arsenal.
Kipa wao nambari mbili, Stuart Taylor, alifanyiwa operesheni ya goti na hajapona na Kipa wao mwingine wa kutumainiwa, Joe Hart, ambae ndie ametajwa kuwa ndio Kipa wa Timu Bora ya Msimu, yuko kwa mkopo kwa Msimu wote huu huko Birmingham na mkataba wake haumruhusu kurudi Klabuni kwake Man City hadi Msimu huu uishe.
Kipa nambari nne, David Gonzalez nae pia majeruhi baada ya kuumia nyonga.
Baada ya kuumia Shay Givens Jumamosi akaingizwa Kipa kutoka Faroe Islands Gunnar Nielsen ambae haaminiki kabisa.
Kipa pekee mwingine Man City wanaweza kumchukua ni Bwana Mdogo Loris Karius anaechezea Timu ya Watoto kwenye Chuo chao cha Mafunzo.
Ancelotti avimba bichwa!!
Baada ya kupata lundo la magoli jana walipoibamiza Stoke City bao 7-0 na kutwaa tena uongozi wa Ligi Kuu wakiwa mbele ya Manchester United kwa pointi moja, Meneja wa Ancelotti amedai hawana presha yeyote na wanajua wakishinda mechi zao mbili zilizobaki wao ni Mabingwa.
Ancelotti amedai: “Tulikuwa na presha kabla ya mechi na Stoke. Lakini sasa hatuna na tunajua tukishinda mechi mbili ni Mabingwa.”
Chelsea Jumapili watakuwa Anfield kuikwaa Liverpool ambao bado wana matumaini ya kuitwaa nafasi ya 4 ya Ligi na hivyo kucheza Ulaya Msimu ujao.
Mechi yao ya mwisho ni Stamford Bridge na Wigan.

No comments:

Powered By Blogger