Sunday 25 April 2010

Blatter aiponda Afrika kutimua Makocha kila kukicha!
Rais wa FIFA, Sepp Blatter, ambae husaidia sana Afrika kisoka, amelaumu vikali tabia ya Nchi za Afrika kubadilisha Makocha kila mara.
Blatter amesema Afrika ina vipaji sawa au zaidi ya Brazil na Nchi za Marekani ya Kusini lakini mbinu hamna na hilo haliwezi kupatikana ikiwa Makocha wanabadilika mara kwa mara na tena hufanyika karibu na Mashindano makubwa.
Afrika ina Nchi 5 kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 11 huko Afrika Kusini na tatu kati ya hizo zimebadilisha Makocha hivi karibuni.
Mwishoni mwa mwezi uliokwisha Ivory Coast ilimteua Kocha wa zamani wa England Sven-Goran Eriksson baada ya kumtimua Vahid Halilhodzic kutoka Bosnia.
Nigeria ilimteua Lars Lagerback kutoka Sweden kumbadili Shaibo Amodu mwezi Februari.
Afrika Kusini nao walimteua Mbrazil Carlos Alberto Parreira mwezi Oktoba mwaka jana baada ya kumfukuza Mbrazil mwingine Joel Santana.
Santana alikuwa kachukua nafasi ya Parreira Aprili 2008 alielazimika kuondoka baada ya kuuguliwa na Mkewe.

No comments:

Powered By Blogger