Sunday 25 April 2010

Chelsea 7 Stoke 0
-Chelsea yarudi kileleni kwa kishindo!!
Wakiwa nyumbani Stamford Bridge, Chelsea leo wameishindilia Stoke City bao 7 na kuipiku Manchester United kileleni.
Zikiwa zimebaki mechi mbili, Chelsea wanaongoza wakiwa na pointi 80 na Manchester United wana pointi 79.
Mechi inayofuata kwa Chelsea ni safari ya Anfield kuivaa Liverpool wakati Manchester United watakuwa Stadium of Light kucheza na Sunderland.
Mechi zote hizo zitakuwa Jumapili Mei mbili.
Mpaka mapumziko Chelsea walikuwa mbele kwa 3-0.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Kalou, bao 3, Lampard bao 2, Sturridge moja na Malouda moja.

No comments:

Powered By Blogger