Friday 30 April 2010

Liverpool washinda lakini nje EUROPA!!!
FAINALI: Fulham v Atletico Madrid Mei 12
Licha ya kushinda bao 2-1 dhidi ya Atletico Madrid, Liverpool walijikuta wakitupwa nje kwa goli la ugenini baada ya jumla ya magoli katika mechi mbili kuwa 2-2 na hivyo Atletico Madrid kutinga Fainali kucheza na Fulham hapo Mei 12 huko Uwanja Nordbank Arena, Hamburg.
Atletico Madrid waliifunga Liverpool bao 1-0 katika mechi ya kwanza kwa bao la Diego Forlan, aliekuwa Mchezaji wa zamani wa Manchester United, na ni Diego Forlan tena aliepachika bao la leo muhimu la ugenini la Atletico.
Hadi dakika 90 za mchezo kumalizika Liverpool walikuwa mbele kwa bao 1-0 kwa bao la dakika ya 44 la Alberto Aquilani lakini matokeo yalikuwa ni 1-1 kwa vile Atletico walishinda mechi ya kwanza bao 1-0 na ndipo dakika 30 za nyongeza zikaanza kutumika.
Liverpool wakapata bao la pili dakika ya 95 kupitia Yossi Benayoun na kuwafanya wawe wanaongoza 2-0 na kama matokeo yangebaki hivi basi ni wao ndio wangetinga Fainali.
Lakini kwenye dakika ya 102, krosi ya Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Antonio Reyes, ilimkuta Diego Forlan yuko peke yake na akapachika bao na kuwapa Atletico bao lao la ugenini lililowapa ushindi baada dakika 120 kumalizika huku Liverpool wakiwa bao 2-1 mbele katika mechi hii.
Vikosi vilikuwa:
Liverpool: Reina, Mascherano, Carragher, Agger, Johnson, Gerrard, Lucas, Benayoun, Aquilani, Babel, Kuyt.
Akiba: Cavalieri, Kyrgiakos, Ngog, Degen, El Zhar, Ayala, Pacheco.
Atletico Madrid: De Gea, Valera, Dominguez, Perea, Antonio Lopez, Reyes, Paulo Assuncao, Raul Garcia, Simao, Aguero, Forlan.
Akiba: Sergio Asenjo, Camacho, Jurado, Salvio, Juanito, Ujfalusi, Cabrera.
Refa: Terje Hauge (Norway)

No comments:

Powered By Blogger