Monday 26 April 2010

Rooney ni Mchezaji wa Mwaka
-Milner aopoa kwa Vijana
-Radebe apewa Tuzo ya Kutukuka
Wayne Rooney amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwaka huko England katika uchaguzi uliofanywa na Wachezaji wa Kulipwa kupitia Chama chao PFA [Professional Footballers Association].
Straika huyo wa Manchester United aliwabwaga Didier Drogba, Carlos Tevez na Cesc Fabregas katika uchaguzi huo.
Rooney, miaka 24, alisema: “Najiskia furaha sana kushinda Tuzo hii kwa sababu nimechaguliwa na Wachezaji wenzangu. Ni heshima kubwa na nasikia fahari mno!”
Msimu huu, Rooney amefunga mabao 34 na ameng’ara sana hasa kwa vile amesogezwa mbele zaidi katika pozisheni ya uchezaji na hilo limemfanya afunge bao nyingi.
Pia kuondoka kwa Ronaldo na Tevez Man United kulimtwisha mzigo mkubwa lakini ameweza kuleta mafanikio makubwa Klabuni kwake.
Katika Tuzo kama hiyo kwa upande wa Wachezaji Vijana, James Milner wa Aston Villa ndie Mshindi.
Nae Mchezaji wa zamani wa Leeds na Bafana Bafana, Lucas Radebe, miaka 41, ametunukiwa Tuzo ya Kutukuka ya PFA kwa kutambua mchango wake mkubwa kwa jamii.
Radebe amezungumza: “Michezo hubadilisha Dunia. Soka imetoa mchango mkubwa kuinua jamii yangu. Nasikia fahari mno kushinda Tuzo hii!”
-TIMU BORA YA LIGI KUU YA MWAKA:
Sambamba na Wachezaji Bora, pia ilichaguliwa Timu Bora na ni kama ifuatavyo huku Klabu za Wachezaji kwenye mabano:
-Kipa: Joe Hart [Man City, yuko kwa mkopo Birmingham]
-Branislav Ivanovic [Chelsea], Thomas Vermaelen [Arsenal], Richard Dunne [Aston Villa], Patrice Evra [Man United], Cesc Fabregas [Arsenal], James Milner [Aston Villa], Darren Fletcher [Man United], Antonio Valencia [Man United], Wayne Rooney [Man United], Didier Drogba [Chelsea].

No comments:

Powered By Blogger