Sunday 25 April 2010

Rangers Mabingwa Scotland
Leo Rangers wamefanikiwa kutetea Taji la Ubingwa wa Scotland walipowalaza Hibernian kwa bao 1-0 Mfungaji akiwa Kyle Lafferty.
Rangers wangeweza kuutwaa Ubingwa mapema leo kama Celtic wangeteleza lakini hao Mahasimu wao wakubwa waliibuka washindi walipowafunga Dundee United bao 2-0 katika mechi iliyoanza mapema kabla ya Rangers.
Burnley waporomoka!
Burnley imekuwa Timu ya pili Msimu huu kushuka Daraja na kuifuata Portsmouth walipotandikwa bao 4-0 na Liverpool Uwanjani Turf Moor.
Burnley walivimba hadi mapumziko bao zikiwa 0-0 lakini kisago chao kikaanza kipindi cha pili Steven Gerrard alipofunga bao mbili dakika ya 52 na 59.
Kisha Maxi Rodriguez akapachika bao la 3 dakika ya 74 na Babel amaliza kwenye dakika za majeruhi.
Liverpool wapo nafasi ya 7 wakiwa pointi mbili tu nyuma ya Tottenham walio nafasi ya 4.
Everton 2 Fulham 1
Penalti ya dakika za majeruhi iliyofungwa na Mikel Arteta imewapa Everton ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Fulham Uwanjani Goodison Park kwenye mechi ya Ligi Kuu.
Fulham walitangulia kupata bao baada ya makosa ya Beki Leighton Baines kutaka kumrudishia Kipa Tim Howard na Erik Nevland akaunasa na kufunga.
Hiyo ilikuwa dakika ya 36.
Kipindi cha pili dakika ya 49, kichwa cha Victor Anichebe kilimgonga Beki Chris Smalling, ambae Msimu ujao atachezea Man United, na kuisawazishia Everton.
Ndipo ngoma ikielekea kulala Chris Baird akamchezea madhambi Tim Cahill na ikaamuliwa penalti.

No comments:

Powered By Blogger