Wednesday 28 April 2010

Ribery kuikosa Fainali UEFA
-Kifungo Mechi 3!!!
Nyota wa Bayern Munich Franck Ribery ataikosa Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI baada ya UEFA kumfungia mechi tatu.
Ribery alipewa Kadi Nyekundu katika mechi ya kwanza kati ya Bayern Munich na Lyon baada ya kumkanyaga Fowadi wa Lyon Lisandro Lopez na jana hakucheza mechi ya marudiano ambayo Bayern walishinda 3-0 na kufuzu kuingia Fainali.
Lakini sasa UEFA imeamua kumfungia mechi 3 baada ya kupitia upya tukio hilo na hivyo Fainali itakuwa mechi yake ya pili ya kifungo chake cha mechi 3.
Bayern Munich imepewa siku tatu kukata Rufaa lakini kwa kawaida kwa UEFA Rufaa huwa zinapiga chini.
Mkongwe amtaka Scholes arudishwe England
Mkongwe Sir Geoff Hurst ambae aliisaidia England kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1966 ametaka Mchezaji wa Manchester United Paul Scholes arudishwe tena Kikosi cha England na amemwomba Meneja wa England Fabio Capello amwite Mchezaji huyo.
Scholes, miaka 35, alieichezea England mara 66, alistaafu kucheza Timu hiyo mwaka 2004.
Lakini Sir Geoff Hurst, aliefunga goli 3 mguuni kwake na kuiua Ujerumani 4-2 katika Fainali ya Kombe la Dunia iliyochezwa Wembley mwaka 1966 na kuifanya England iwe Bingwa wa Dunia, amemtaka Capello amwite Scholes kwenye Kikosi chake na amedai hilo litaongeza uwezo wa England kunyakua Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.

No comments:

Powered By Blogger