Friday 30 April 2010

Fulham Fainali EUROPA
Wakiwa nyuma kwa bao 1-0 hadi mapumziko, kwa bao la frikiki ya mita 30 iliyopigwa na Petric na kutinga moja kwa moja wavuni, Fulham wakiwa nyumbani kwao Craven Cottage walijikakamua na kufunga bao mbili kipindi cha pili na kutinga Fainali ya Kombe la EUROPA mahsusi kwa jina la EUROPA LIGI, hii ikiwa ni Fainali yao ya kwanza katika Ulaya.
Timu hizi zilitoka sare 0-0 katika mechi ya kwanza huko Hamburg, Ujerumani wiki iliyokwisha.
Mfungaji mkuu wa Fulham Bobby Zamora, aliekuwa na hatihati kucheza mechi hii kwa kuwa majeruhi, alianza mechi hii na nusura aipatie Timu yake bao lakini Kipa wa Hamburg Frank Rost aliokoa.
Ndipo Hamburg wakafunga bao kutokana na frikiki ya Mladen Petric ya mita 30 iliyoenda moja kwa moja juu wavuni.
Hiyo ilikuwa dakika ya 22.
Dakika ya 69 ya mchezo pasi ndefu toka Defensi ilimkuta Simon Davies aliemgeuza Beki Guy Durnel na kuachia kigongo kufanya bao ziwe 1-1.
Kona ya Simon Davies kwenye dakika ya 76 ilimkuta Zoltan Gera aliemalizia na kufunga bao la pili na la ushindi ni lililowapeleka Fulham Fainali ya EUROPA LIGI itakayochezwa Uwanja wa Timu waliyoifunga, Hamburg, uitwao Nordbank Arena hapo Mei 12.
Vikosi vilikuwa:
Fulham: Schwarzer, Pantsil, Hangeland, Hughes, Konchesky, Davies, Murphy, Etuhu, Duff, Gera, Zamora.
Akiba: Zuberbuhler, Nevland, Riise, Dempsey, Smalling, Greening, Dikgacoi.
Hamburg: Rost, Aogo, Mathijsen, Boateng, Demel, Pitroipa, Ze Roberto, Jarolim, Tesche, Petric, van Nistelrooy.
Akiba: Hesl, Rozehnal, Guerrero, Berg, Arslan, Rincon, Schulz.
Refa: Cuneyt Cakir (Turkey)

No comments:

Powered By Blogger