Saturday 24 April 2010

Ze Gunners kwisha kazi!!!
-Msimu mwingine tena patupuuuuu!!!
Leo wakiwa kwao Emirates, Arsenal rasmi wamemaliza matumaini yao ya kutwaa Ubingwa na kupata Kikombe cha kwanza tangu 2005 walipotoka sare 0-0 na Manchester City kwenye mechi ya Ligi Kuu.
Kwa sare ya leo, Arsenal wamefikisha pointi 72 na wamebakisha mechi mbili wakati Man United wanaoongoza Ligi tayari wana pointi 79.
Pia, sare hii ya leo imewafanya Man City wang’ang’anie nafasi ya 5 pointi moja nyuma ya Tottenham waliofungwa mechi ya awali leo na Man United bao 3-2.
Mechi ya leo ni rahisi kuisahau kwa kukosa msisimko wowote labda kuzomewa kwa Emmanuel Adebayor wa Man City alieingizwa kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Patrick Viera ambae alikuwa akishangiliwa na Washabiki wa Arsenal.
Arsenal: Fabianski, Sagna, Campbell, Silvestre, Clichy, Song, Diaby, Walcott, Nasri, Rosicky, van Persie.
Vikosi vilivyoanza:
Akiba: Mannone, Eduardo, Vela, Eboue, Traore, Eastmond, Bendtner.
Man City: Given, Zabaleta, Toure, Kompany, Bridge, De Jong, Vieira, Barry, Adam Johnson, Bellamy, Tevez.
Akiba: Nielsen, Richards, Onuoha, Ireland, Wright-Phillips, Santa Cruz, Adebayor.
Refa: Mike Dean

No comments:

Powered By Blogger