Monday 19 April 2010

Ligi Kuu basi kwa Torres
Mshambuliaji wa Liverpool Fernando Torres ameshaiaga Ligi Kuu Msimu huu pale alipofanyiwa upasuaji wa goti lake siku ya Jumapili na Madaktari wanasema kupona atachukua wiki 6 na hii ina maana hawezi kucheza tena Ligi kwa vile inamalizika Mei 9.
Hata Timu yake ya Taifa Spain itakuwa ikimtazama kwa wasiwasi kwani Timu zinatakiwa kuwasilisha kwa FIFA Listi zao za mwisho za Wachezaji 23 Juni 1.
Kwenye Ligi Kuu, Liverpool bado ina nafasi finyu ya kuipata nafasi ya 4 itakayowawezesha kucheza Ulaya Msimu ujao.
Alhamisi, Liverpool wapo Spain kucheza mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya EUROPA LIGI na Atletico Madrid.
Pompey 1 Villa 2
Nathan Delfouneso aliingizwa kama Mchezaji wa Akiba kipindi cha pili na kufunga bao la ushindi kwa Aston Villa dhidi ya Portsmouth ambayo tayari ishashuka Darajana kuyaweka hai matumaini ya kuipata nafasi ya 4 kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu iliyochezwa Fratton Park, Pompey walikuwa wa kwanza kupata bao Mfungaji akiwa Michael Brown dakika ya 10 na Villa wakasawazisha kwa bao la John Carew dakika ya 16.
Papa Bouba Diop akawapa Villa zawadi pale chenga zake ndani ya boksi zilipomfanya acheze rafu aliponyang’anywa mpira na kutolewa penalty ambayo ilipigwa na John Carew lakini Kipa wa Pompey David James akapangua.
Dakika ya 82 ndipo Delfouneso akafunga bao la pili na la ushindi na kuwafanya Villa wafikishe pointi 58 wakiwa nafasi ya 6, juu yao wapo Man City wenye pointi 62 na Spurs wako nafasi ya 4 wakiwa na pointi 64.
Timu hizi zote zimebakisha mechi 4.

No comments:

Powered By Blogger