Thursday 22 April 2010

NUSU FAINALI: Leo Atletico Madrid v Liverpool & Hamburger SV v Fulham
Baada ya kusafiri kwa ‘Madaladala’ hadi Spain na Ujerumani, leo usiku Timu za Liverpool na Fulham ziko ugenini kucheza mechi za kwanza za Nusu Fainali za EUROPA LIGI wakati Liverpool atakapomenyana na Atletico Madrid na Fulham wataivaa Hamburger.
Marudio ya mechi hizo ni Alhamisi ijayo Aprili 29.
Bayern Munich 1 Lyon 0
Wakiwa kwao Uwanja wa Allianz Arena, Bayern Munich walimpoteza Staa wao Franck Ribery aliewashwa Kadi Nyekundu na Refa kutoka Italia Roberto Rosetti baada ya kumtimba Cris kwenye dakika ya 37 lakini wakaibuka washindi kwa shuti la Staa wao mwingine Arjen Robben lililomparaza Muller kichwani na kumbabaisha Kipa Lloris na kutinga wavuni kwenye dakika ya 69 kuwapa Bayern ushindi wa bao 1-0.
Lyon pia walimpoteza Mchezaji wao Toulalan aliepewa Kadi mbili za Njano na kutolewa dakika ya 54 lakini walinusurika athari zaidi ya kukosa Wachezaji kwenye mechi ya marudiano wiki ijayo baada ya Wachezaji wao wengine kukwepa Kadi kwani walikuwa na Wachezaji 7 tayari wana Kadi na kama wangepata Kadi ya Njano wasingecheza marudiano.
Vikosi vilivyoanza:
Bayern Munich: Butt, Lahm, Van Buyten, Demichelis, Contento, Robben (Altintop 85), Schweinsteiger, Pranjic (Gomez 63), Ribery, Muller, Olic (Tymoschuk 46).
Akiba hawakucheza: Rensing, Gorlitz, Klose, Alaba.
Lyon: Lloris, Reveillere, Cris, Toulalan, Cissokho, Gonalons, Kallstrom, Ederson (Michel Bastos 71), Pjanic (Makoun 55), Delgado (Govou 79), Lopez. Akiba hawakucheza: Vercoutre, Gomis, Anderson, Gassama.
Hull City 0 Aston Villa 2
Aston Villa wameendelea kuweka hai matumaini yao ya kunyakua nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu walipoichapa Hull City bao 2-0 kwenye Uwanja wa KC.
Bao la kwanza la Villa lilipatikana dakika ya 13 baada ya Beki Paul McShane kuokoa butu na mpira kumfikia Straika wa Villa John Carew aliemsogezea Gabriel Agbonlahor na kufunga.
James Milner akaipatia Villa bao la pili kwa penalti dakika ya 76 baada ya yeye mwenyewe kuangushwa na George Boateng.
Obi kwaheri Msimu!!!
Kiungo wa Chelsea kutoka Nigeria, John Obi Mikel, yumo hatarini kuzikosa mechi zilizobaki za Ligi Kuu Msimu huu baada ya kuumia goti na kuambiwa anahitaji wiki 3 ili kupona.
Obi alitoka nje dakika ya 33 huko White Hart Lane Chelsea walipofungwa na Tottenham 2-1 wikiendi iliyokwisha na kubadilishwa na Michael Ballack.
Mechi zinazofuata za Chelsea za Ligi Kuu ni Jumapili watakapocheza na Stoke City, tarehe 1 Mei na Liverpool na tarehe 9 Mei, Ligi itakapokwisha, watamaliza na Wigan.
Mei 15, Chelsea wapo Wembley kucheza Fainali ya FA Cup na Portsmouth.

No comments:

Powered By Blogger