Friday 23 April 2010

Mchezaji wa Man United awaua Liverpool!!
Atletico Madrid 1 Liverpool 0
Mchezaji wa zamani wa Manchester United, Diego Forlan, alifunga bao dakika ya 9 na kuihakikishia Atletico Madrid ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Liverpool kwenye mechi ya kwanza ya EUROPA LIGI iliyochezwa Uwanjani Vicente Calderon Mjini Madrid, Spain.
Liverpool walionekana wachovu pengine ni sababu ya safari ya umbali wa maili 1200 kwa njia za Treni, Basi na Ndege kutokana na balaa la Majivu ya Volcano ya huko Iceland.
Timu hizi zitarudiana Anfield Alhamisi ijayo Aprili 29.
Ingawa Atletico Madrid wameshinda lakini pengine watajuta kwa kukosa bao kadhaa za wazi na labda kumkosa kwa Straika wao mwingine, Kun Aguero kutoka Argentina, kumechangia hilo.
Aguero hakucheza kwa vile kafungiwa lakini mechi ijayo yupo huru kucheza.
Nao Liverpool walionekana wazi pengo la Fernando Torres, ambae ni Mchezaji wa zamani wa Atletico Madrid, linawaletea kasoro.
Pia, katika mechi nzima Mawinga wa Atletico, Simao na Antonio Reyes, Mchezaji wa zamani wa Arsenal, waliwachachafya sana.
Vikosi vilikuwa:
Atletico Madrid: De Gea, Antonio Lopez, Ujfalusi, Dominguez, Perea, Raul Garcia, Paulo Assuncao, Simao [Valera 77], Forlan [Eduardo Salvio] 85], Jurado, Reyes [Camacho 90].
Liverpool: Reina, Johnson, Agger, Kyrgiakos, Carragher, Gerrard, Benayoun [El Zhar], Mascherano, Lucas, Kuyt, Ngog [Babel 64]
Hamburg 0 Fulham 0
Kwenye Nusu Fainali nyingine ya EUROPA LIGI, Fulham wakicheza ugenini huko Ujerumani walimudu kutofungwa na Hamburg na hivyo kujiweka katika nafasi nzuri Timu hizi zitakaporudiana huko Craven Cottage Alhamisi ijayo Aprili 29.
Fulham, wakicheza fomesheni ya 4-5-1 huku Bobby Zamora akiwa ndie Straika pekee mbele, walipata pigo pale Zamora alipoumia na kutolewa dakika ya 52 na kuingizwa Clint Dempsey.
Nao Hamburg, walikosa bao pale Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Ruud van Nistelrooy, aliposhindwa kufunga.
Katika mechi yote, Fulham walisimama ngangari katika ulinzi.
Vikosi vilikuwa:
Hamburg: Rost, Mathijsen, Boateng, Demel [Rincon 82], Aogo, Ze Roberto, Jarolim, Trochowski, Pitroipa, Guerrero [Petric 72], Ruud van Nistelrooy
Fulham: Schwarzer, Konchesky, Hangeland, Baird, Hughes, Gera, Murphy, Duff, Etuhu, Davies, Zamora [Dempsey 52]

No comments:

Powered By Blogger