Atletico Madrid 1 Liverpool 0

Timu hizi zitarudiana Anfield Alhamisi ijayo Aprili 29.
Ingawa Atletico Madrid wameshinda lakini pengine watajuta kwa kukosa bao kadhaa za wazi na labda kumkosa kwa Straika wao mwingine, Kun Aguero kutoka Argentina, kumechangia hilo.
Aguero hakucheza kwa vile kafungiwa lakini mechi ijayo yupo huru kucheza.
Nao Liverpool walionekana wazi pengo la Fernando Torres, ambae ni Mchezaji wa zamani wa Atletico Madrid, linawaletea kasoro.
Pia, katika mechi nzima Mawinga wa Atletico, Simao na Antonio Reyes, Mchezaji wa zamani wa Arsenal, waliwachachafya sana.
Vikosi vilikuwa:
Atletico Madrid: De Gea, Antonio Lopez, Ujfalusi, Dominguez, Perea, Raul Garcia, Paulo Assuncao, Simao [Valera 77], Forlan [Eduardo Salvio] 85], Jurado, Reyes [Camacho 90].
Liverpool: Reina, Johnson, Agger, Kyrgiakos, Carragher, Gerrard, Benayoun [El Zhar], Mascherano, Lucas, Kuyt, Ngog [Babel 64]
Hamburg 0 Fulham 0

Nao Hamburg, walikosa bao pale Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Ruud van Nistelrooy, aliposhindwa kufunga.
Katika mechi yote, Fulham walisimama ngangari katika ulinzi.
Vikosi vilikuwa:
Hamburg: Rost, Mathijsen, Boateng, Demel [Rincon 82], Aogo, Ze Roberto, Jarolim, Trochowski, Pitroipa, Guerrero [Petric 72], Ruud van Nistelrooy
Fulham: Schwarzer, Konchesky, Hangeland, Baird, Hughes, Gera, Murphy, Duff, Etuhu, Davies, Zamora [Dempsey 52]
No comments:
Post a Comment