Saturday 24 April 2010

Rooney nje mechi za Man United
Straika wa Manchester United Wayne Rooney huenda akazikosa mechi za Timu yake zilizobaki za Msimu huu baada ya kuumia nyonga mazoezini siku ya Alhamisi lakini atakuwa fiti kuichezea England kwenye Fainali za Kombe la Dunia.
Habari za kuumia kwake zimethibitishwa na Kocha wake Sir Alex Ferguson na leo hakucheza kwenye ushindi wa 3-1 dhidi ya Tottenham kwenye mechi ya LigI Kuu.
Hivi karibuni Rooney amekuwa akikumbwa na majeruhi na aliumizwa kwenye mechi zote mbili za Robo Fainali za UEFA CHAMPIONS LIGI Man United walipocheza na Bayern Munich.
Mechi za Man United za Ligi Kuu zilizobaki ni za wiki ijayo na Sunderland na ya mwisho ni Mei 9 na Stoke City.
Kwa England, Rooney, ambae ameifungia Klabu yake bao 34 Msimu huu na England bao 8, ni ufunguo wa mafanikio yao.
England itacheza mechi za kirafiki na Mexico Mei 24 Uwanjani Wembley na Japan huko Graz, Austria Mei 30.
Mechi ya kwanza kwa England kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini ni Juni 12 dhidi ya USA Mjini Rustenburg.

No comments:

Powered By Blogger