Wednesday 21 April 2010

Inter Milan 3 Barcelona 1
Inter Milan, wakiwa bao moja nyuma, walifanikiwa kuilaza Barcelona mabao 3-1 Uwanjani San Siro kwenye mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Barca walipata bao lao kupitia Pedro baada ya krosi ya Maxwell.
Inter walisawazisha pale Wesley Sneijder alipofunga kufuatia pasi ya Diego Milito na ni Milito tena aliemtengenezea Maicon kufunga bao la pili.
Na ni Milito alieifungia Inter bao la 3.
Katika mechi hii Inter walimudu kuwabana Barca ambao nyota wao Lionel Messi alionekana kupwaya.
Mechi ya marudiano ni wiki ijayo Aprili 28 huko Nou Camp.
Leo ni Nusu Fainali ya pili kati ya Bayern Munich na Lyon.

No comments:

Powered By Blogger