Saturday 24 April 2010

Maporomoko yawanukia Hull, West Ham wajinasua polepole!!!!
MATOKEO LIGI KUU:
Jumamosi, 24 Aprili 2010
Man United 3 v Tottenham 1
Bolton 2 v Portsmouth 2
Hull 0 v Sunderland 1
West Ham 3 v Wigan 2
Wolves 1 v Blackburn 1
West Ham 3 Wigan 2
West Ham leo wamegangamara katika vita yao kujihakikishia wanabaki Ligi Kuu walipowafunga Wigan, Timu nyingine ambayo pia bado haijapona, kwa bao 3-2.
West Ham waliianza mechi hii kwa balaa baada ya Beki wao Jonathan Spector kujifunga mwenyewe kwenye dakika ya 4 tu. Lakini dakika ya 31 Ilan akasawazisha kufuatia krosi ya Carlton Cole na Radoslav Kovac akawapachikia West Ham bao la pili dakika ya 45.
Wigan wakaifanya gemu iwe 2-2 kupitia Rodallega kwenye dakika ya 52.
Scott Parker, Kiungo anaeibeba West Ham karibu kila mechi, ndie aliekuwa mkombozi alipofunga bao la ushindi dakika ya 77 kwa kigongo kutoka mita 25.
Kutokana na matokeo haya na pia leo Hull City kuchapwa 1-0 na Sunderland, huku kukiwa kumebaki mechi mbili tu, West Ham sasa wako pointi 6 juu ya Hull City walio Timu ya 3 toka mkiani na hivyo wana nafasi kubwa kupuruchuka kushushwa Daraja balaa ambalo linawakabili Hull City na Burnley ilio chini ya Hull.
Chini ya Hull na Burnley, kwenye nafasi ya mwisho, wapo Portsmouth ambao tayari washashuka Daraja.
Ikiwa kesho Burnley watafungwa na Liverpool, West Ham na Wigan watapata uhakika wa kubaki Ligi Kuu.
Hull City 0 Sunderland 1
Hull City walikosa penalti, Mchezaji wao Jozy Altidore, pamoja na Alan Hutton wa Sunderland, walitolewa kwa Kadi Nyekundu na wakafungwa bao 1-0 na hivyo safari ya kwenda kucheza Daraja la chini imeanza kuiva hasa baada ya Timu iliyo juu yao West Ham kuifunga Wigan 3-2 na kufanya pengo kati yao kuwa pointi 6 huku mechi zimebaki mbili tu.
Kichwa cha Darren Bent baada ya pasi ya Kenwyne Jones dakika ya 7 ndio kimewaua Hull City.

No comments:

Powered By Blogger