Sunday 18 April 2010

Ze Gunners watwangwa!!!
Dakika 10 za mwisho zilizaa mabao matatu ya Wigan waliokuwa nyuma kwa bao mbili na kuweza kuitwanga Arsenal bao 3-2 na kuifanya Arsenal ipoteze matumaini ya Ubingwa.
Theo Walcott aliipa Arsenal bao la kwanza na Mikael Silvestre akapachika bao la pili kwa kichwa kufuatia kona.
Lakini Wigan ambao bado walikuwa kwenye wimbi la hatari ya kushuka walijitutumua na katika dakika 10 za mwisho wakafunga bao 3.
Ben Watson akaipatia Wigan bao la kwanza na Kipa wa Arsenal Lukasz Fabianski akafanya uzembe uliomruhusu Titus Bramble kupiga kichwa na kufunga.
Kwenye dakika za majeruhi huku bao zikiwa 2-2, Charles N’Zogbia akafumua fataki nje ya boksi na mpira kugonga mwamba na kutinga wavuni.
Bao hilo pengine ndio limeua matumaini yote ya Arsenal ya kutwaa Ubingwa kwani wamekwama wakiwa nafasi ya 3, mechi zimebaki 3 na wana pointi 71.
Juu yao wapo Manchester United wenye pointi 76 na Chelsea ndio vinara wenye 77 na Timu zote hizo zimebakisha mechi 3.

No comments:

Powered By Blogger