Saturday 24 April 2010

LIGI KUU: NDOTO ZA FISI????
Ukiachia Timu chache, Timu nyingi kwenye Ligi Kuu zimebakisha mechi 3 kumaliza Ligi na kileleni wapo Chelsea walio mbele ya Manchester United kwa pointi moja tu.
Nyuma ya Man United wapo Arsenal walio pointi 5 nyuma.
Kimahesabu, ni Chelsea, Man United na Arsenal ndizo zinaweza kutwaa Ubingwa ingawa nafasi kubwa ni ya Chelsea kwa vile tu yuko pointi moja mbele na akishinda mechi zake 3 zilizobaki ni Bingwa.
Hivyo, kwa Man United na Arsenal, ni ile hadithi ya Fisi kuufuata mkono wa Binadamu kungoja udondoke.
Lakini ni nani anajua kama ipo siku utadondoka?
RATIBA:
[Saa za Bongo]
_____________________________________
Jumamosi, 24 Aprili 2010
[saa 8 dak 45 mchana]
Man United v Tottenham
[saa 11 jioni]
Bolton v Portsmouth
Hull v Sunderland
West Ham v Wigan
Wolves v Blackburn
[saa 1 na nusu usiku]
Arsenal v Man City
________________________________________
Jumapili, 25 Aprili 2010
[saa 8 mchana]
Aston Villa v Birmingham
[saa 11 jioni]
Burnley v Liverpool
Everton v Fulham
[saa 12 jioni]
Chelsea v Stoke
------------------------------------------------
MSIMAMO LIGI KUU
[Aprili 24]:
1. Chelsea mechi 35 pointi 77
2. Man United mechi 35 pointi 76
3. Arsenal mechi 35 pointi 71
4. Tottenham mechi 34 pointi 64
5. Man City mechi 34 pointi 62
6. Aston Villa mechi 35 pointi 61
7. Liverpool mechi 35 pointi 59
8. Everton mechi 35 pointi 54
9. Birmingham mechi 35 pointi 47
10.Fulham mechi 34 pointi 43
11.Stoke mechi 34 pointi43
12.Blackburn mechi 35 pointi 43
13.Sunderland mechi 35 pointi 41
14.Bolton mechi 35 pointi 35
15.Wigan mechi 35 pointi 35
16.Wolves mechi 35 pointi 34
17.West Ham mechi 35 pointi 31
18.Hull mechi 35 pointi 28
19.Burnley mechi 35 pointi 27
20.Portsmouth mechi 35 pointi 15
MECHI ZA JUMAMOSI:
Manchester United v Tottenham
Baada ya kuzitandika Chelsea na Arsenal ndani ya siku 4, Tottenham wako safarini hadi Old Trafford kuwakwaa Mabingwa Watetezi Manchester United na hii ni mechi yenye uzito mkubwa kwa Timu zote mbili.
Man United wakishinda watachukua uongozi wa Ligi Kuu japo kwa masaa 24 tu ikiwa Chelsea atashinda mechi yake ya Jumapili atakapocheza na Stoke City.
Tottenham, walio nafasi ya 4 pointi 2 mbele ya Manchester City, wanataka kuendeleza ushindi ili wajikite vizuri nafasi hiyo itakayowapeleka Ulaya Msimu ujao.
Lakini, Man United wana rekodi nzuri ya kutofungwa Old Trafford na Tottenham kwenye Ligi Kuu na wameshinda mechi 14 kati ya 17 walizocheza pamoja.
Katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Msimu huu, Man United waliifunga Tottenham 3-1 huko White Hart Lane.
Arsenal v Man City
Mara nyingi Arsenal wakikumbana na kipigo, huibuka na kupata ushindi mnono lakini kile kipigo cha Wigan cha dakika 10 za mwisho kiliwastua wengi na Jumamosi wanakutana na Man City Timu inayowania nafasi ya 4 na yenye Wachezaji kadhaa waliotokea Arsenal kama vile Adebayor, Kolo Toure na Viera.
Mbali ya wachezaji hao wa zamani wa Arsenal, pia mechi hii inangojewa kwa hamu kwa vile Man City waliitwanga Arsenal 4-2 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Msimu huu.
Hull City v Sunderland
Hull City wako kwenye balaa la kushushwa Daraja wakiwa Timu ya 3 toka mkiani na wanakutana na Sunderland Timu ambayo tayari imepona balaa hilo.
Zikiwa zimebaki mechi 3 tu ni dhahiri mechi zinakwisha haraka kwa Hull kujinusuru.
West Ham v Wigan
Kudidimia kwa Hull City kumewapa ahueni kidogo West Ham walio pointi 3 mbele ya Hull na pambano lao na Wigan ni mechi muhimu kwao na pia kwa Wigan ambao kidogo walipata afueni walipoifunga Arsenal kimiujiza mechi ya wikiendi iliyopita.
Wolves v Blackburn
Ushindi kwa Wolves katika mechi hii na Blackburn utawahakikishia wanabaki Ligi Kuu.
Bolton v Portsmouth
Kwa Bolton, ushindi kwenye mechi hii dhidi ya Portsmouth ambayo tayari imeshashushwa, una maana watabaki Ligi Kuu.
MECHI ZA JUMAPILI:
Chelsea v Stoke City
Chelsea wako nyumbani Stamford Bridge kucheza na Stoke siku ya Jumapili na inawezekana wakati wanaanza mechi hii Man United atakuwa kileleni ikiwa watamfunga Tottenham siku ya Jumamosi.
Stoke wanaingia kwenye mechi hii bila ya woga wowote kwa vile wako salama kwenye Ligi Kuu.
Aston Villa v Birmingham
Hii ni dabi ya Timu za Midlands na Aston Villa bado wana matumaini ya kunyakua nafasi ya 4 ingawa kidogo iko mbali kwao kwani wako nafasi ya 6 pointi 3 nyuma ya Tottenham na wamecheza mechi moja zaidi.
Birmingham wao wanaelea tu kwenye Ligi Kuu na mechi hii kwao ni ya kulinda heshima kwa vile ni dabi.
Burnley v Liverpool
Baada ya safari ndefu ya ardhini hadi huko Spain walipofungwa 1-0 na Atletico Madrid kwenye Nusu Fainali ya EUROPA LIGI, Liverpool wanasafiri hadi Turf Moor kucheza na Burnley ambao wako nafasi moja toka mkiani.
Liverpool wako nafasi ya 7 na kimahesabu bado wako kwenye kinyang’anyiro cha nafasi ya 4.
Everton v Fulham
Uwanjani Goodison Park, Everton wanaikaribisha Fulham ambayo ndio kwanza imerudi toka Ujerumani walikotoka droo 0-0 na Hamburg kwenye Nusu Fainali ya EUROPA LIGI.

No comments:

Powered By Blogger