Saturday 24 April 2010

Man United wadandia kilele!!!!
Katika mechi ya Ligi Kuu iliyoanza mapema leo, Manchester United wakiwa kwao Old Trafford, wamemudu kuwabamiza Wababe wa Chelsea na Arsenal, Tottenham, kwa bao 3-1 na kutwaa uongozi wa Ligi wakiwa pointi 2 mbele ya Chelsea ambao wanacheza kesho na Stoke City.
Wakicheza bila ya Mfungaji wao mkuu, Wayne Rooney, Manchester United walifunga bao zao 3 kipindi cha pili.
Bao la kwanza lilifungwa kwa penalti na Ryan Giggs baada ya Beki wa Spurs Assou-Ekotto kumkata Evra aliekuwa akichanja mbuga kufuatia pande la kisigino toka kwa Berbatov.
Hii ilikuwa dakika ya 58.
Tottenham walisawazisha dakika ya 70 baada ya kona ya Bale kumaliziwa kwa kichwa na Ledley King.
Kwenye dakika ya 82, gonga tamu kati ya Darren Fletcher, Kiko Macheda, alieingia kuchukua nafasi ya Rafael,na Nani ilimaliziwa kwa ufundi wa hali ya juu na Nani alieubetua mpira kwa ustadi mkubwa kumpita Kipa Gomes na kuandika bao la pili.
Man United wakapata penalti yao ya pili dakika ya 85 baada ya Wilson Palacios kumuangusha Nani ndani ya boksi na Refa Andre Marriner kuamua ni penalti.
Mkongwe Ryan Giggs, kwa utulivu mkubwa, akaupachika mpira kulia mwa Kipa Gomes na kuifanya Man United iwe mbele kwa bao 3-1.
Vikosi vilivyoanza:
Man United: Van der Sar, Rafael Da Silva, Vidic, Jonathan Evans, Evra, Fletcher, Scholes, Giggs, Valencia, Berbatov, Nani.
Akiba: Kuszczak, Hargreaves, Brown, Carrick, O'Shea, Macheda, Gibson.
Tottenham: Gomes, Assou-Ekotto, Dawson, King, Bale, Bentley, Huddlestone, Palacios, Modric, Defoe, Pavlyuchenko.
Akiba: Alnwick, Kaboul, Lennon, Jenas, Crouch, Gudjohnsen, Bassong.
Refa: Andre Marriner

No comments:

Powered By Blogger