Sunday 18 April 2010

MAJIVU KUTIBUA MECHI ZA ULAYA WIKI HII?
Ulaya imekumbwa na balaa la majivu yatokayo kwenye Volcano iitwayo Eyjafjallajoekul ya huko Iceland na kutapakaa Nchi kadhaa huko Ulaya na kusababisha kusimama kwa safari za Ndege kwa vile majivu hayo huzidhuru Ndege na hatari kubwa ni kuweza kuzifanya Injini za Ndege kuzimika.
UEFA imekuwa ikifuatalia matatizo hayo kwa karibu kwani wiki hii ipo michuano ya Ulaya nayo ni ile ya Nusu Fainali za UEFA CHAMPIONS LIGI Siku za Jumanne na Jumatano.
Alhamisi ni Nusu Fainali za EUROPA LIGI.
Barcelona watasafiri hadi Italia kwa barabara kucheza na Inter Milan kwenye mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI siku ya Jumanne na Jumatano Timu ya Ufaransa Lyon watakuwa Ujerumani kucheza na Bayern Munich na wataenda huko kwa usafiri wa barabara.
Lakini mechi za EUROPA LIGI za Nusu Fainali za Liverpool na Fulham ndizo zenye matatizo makubwa ya usafiri kwani Liverpool wanatakiwa kusafiri hadi Spain kucheza na Atletico Madrid na Fulham wanatakiwa kwenda Ujerumani kucheza na Hamburg.

No comments:

Powered By Blogger