Sunday 18 April 2010

Wenger awaka!
Baada ya kipigo cha bao 3-2 toka kwa Wigan wakiwa wanaongoza 2-0 na dakika zikiwa zimebaki 10, Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, amehuzunishwa na kukasirishwa na kushindwa mechi hiyo ya Ligi Kuu iliyowapotezea matumaini ya kuuonja Ubingwa.
Wenger alilalamika: “Siwezi kusema jinsi kushindwa huko kunavyokera!”
Wenger pia alikiri Kipa wake Fabianski alikuwa na makosa alipofungwa bao la pili lililofanya mechi iwe 2-2.
Wenger alikubali kuwa, kimahesabu, hata Manchester City na Tottenham, zinaweza kuwakuta na kuwapiku kutoka nafasi ya 3 na hivyo ni muhimu kwao kushinda mechi inayofuata.
Alipoulizwa nani sasa atakuwa Bingwa kati ya Chelsea na Manchester United, Wenger alijibu kimkato: “Haipo akilini na wala sijali! Ninachojua ni kwamba tungeshinda leo bado tungekuwa kwenye kinyang’anyiro cha Ubingwa!”

No comments:

Powered By Blogger