Friday 23 April 2010

Man United ni KLABU TAJIRI!!!
Gazeti kubwa lenye hadhi, kusifika na kutambulika Ulimwenguni kote katika masuala ya biashara, Forbes, limetoa listi ya Klabu za Soka Tajiri Duniani na Manchester United ndio inaongoza ikifuatiwa na Real Madrid.
Forbes imetoa thamani ya Man United kuwa ni Pauni Bilioni 1.19, Real Madrid Pauni Milioni 859 na Arsenal, wakiwa nafasi ya 3, Pauni Milioni 767.
Forbes katika kutathmini hutumia takwimu zinazotokana na haki za matangazo, udhamini na mauzo ya tiketi na bidhaa mbalimbali za Klabu.
Katika listi hiyo ya Forbes yenye Timu 20, Barcelona iko nafasi ya 4 na zipo Klabu za Ligi Kuu England 6 pamoja na Newcastle United iliyocheza Daraja la Chini la Coca Cola Championship Msimu huu.
Katika 10 Bora pia zipo Chelsea, Liverpool na AC Milan ingawa thamani za Klabu hizo zimeporomoka kidogo.
LISTI KAMILI:
1. Manchester United
2. Real Madrid
3. Arsenal
4. Barcelona
5. Bayern Munich
6. Liverpool
7. AC Milan
8. Juventus
9. Chelsea
10. Inter Milan
11. Schalke 04
12. Tottenham Hotspur
13. Olympique Lyonnais
14. Hamburg SV
15. AS Roma
16. Werder Bremen
17. Olympique Marseille
18. Borussia Dortmund
19. Manchester City
20. Newcastle United

No comments:

Powered By Blogger