Wednesday 21 April 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Leo Bayern Munich v Lyon
Leo usiku, huko Munich, Ujerumani Uwanja wa Allianz Arena, Wababe wa Manchester United, Bayern Munich, watakuwa dimbani kuwakwaa Lyon ya Ufaransa katika mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya pili ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Jana, Inter Milan waliifunga Barcelona 3-1 katika Nusu Fainali nyingine.
Kutokana na tatizo la usafiri wa anga lililoikumba Ulaya kufuatia Majivu ya Volcano iliyolipuka huko Iceland, Lyon ilibidi waazime ‘Vipanya’ 10 ili wasafirie kwenda Ujerumani.
Wenyeji Bayern Munich watawakosa Wachezaji wao Mark van Bommel na Holger Badstuber ambao wana Kadi.
Lyon watawakosa majeruhi Jean Makoun, Mathieu Bodmer na Jean-Alain Boumsong.
Pia, Lyon watacheza mechi hii huku Wachezaji wao 7 wako hatarini kuikosa mechi ya marudiano Aprili 27 endapo leo watapata Kadi za Njano.
LIGI KUU England: Leo ni Hull City v Aston Villa
Hull City, ambao wako taabani kwenye eneo la kushushwa Daraja wakiwa pointi 3 nyuma ya Timu zilizo salama, leo wako nyumbani kucheza na Timu ngumu Aston Villa kwenye mechi pekee ya Ligi Kuu.
Hull City wana mechi moja mkononi ukilinganisha na Timu zilizoizunguka na hilo huenda likawapa motisha zaidi ili leo wajitutumue.
Aston Villa wako pointi 6 nyuma ya Timu ya 4, Tottenham, na kimahesabu wanaweza wakainyaka nafasi hiyo inayogombewa pia na Manchester City na Liverpool ili kucheza Ulaya Msimu ujao.
Vikosi vinaweza kuwa:
Hull City: Myhill, McShane, Sonko, Mouyokolo, Dawson, Fagan, Cairney, Bullard, Boateng, Kilbane, Vennegoor of Hesselink.
Aston Villa: Friedel, Cuellar, Dunne, Collins, Warnock, Downing, Milner, Petrov, Ashley Young, Carew, Agbonlahor.

No comments:

Powered By Blogger