Thursday 22 April 2010

Mchezaji alieiua Arsenal akamatwa!!
Mchezaji wa Wigan Charles N'Zogbia amekamatwa kwa madai kuwa alimkodi Mtu mwingine amfanyie Testi yake ya nadharia ya kupata Leseni ya Kuendesha Gari.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 mwenye Uraia wa Ufaransa lakini mwenye asili ya Congo alikamatwa na Polisi mara baada ya kuwasili kwenye Kituo cha kufanyia Testi ya Vitendo.
N’Zogbia yuko nje kwa dhamana hadi Juni 3.
Jumapili iliyopita N’Zogbia ndie alieifungia Wigan bao la 3 na la ushindi dakika za majeruhi na kuiua Arsenal 3-2.
Meneja wa Wigan Roberto Martinez amesema: “Nadhani ni kosa la kijinga! Tutaangalia kila kitu na kujua nini tumsaidie!”
Liverpool wataka bao la ugenini huko Vicente Calderon
Liverpool leo wako huko Spain Uwanja wa Vicente Calderon kuivaa Atletico Madrid katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya EUROPA LIGI na Meneja wao Rafa Benitez anahisi ni muhimu kufunga bao la ugenini.
Liverpool waliwasili Madrid kwa njia ya mzunguko wakitumia Basi, Treni na Ndege kwa hatua ya mwisho kufuatia kusimama kwa safari za Ndege kwa sababu ya mlipuko wa Volcano ya Iceland iliyosambaza Majivu.
EUROPA LIGI ndio nafasi ya mwisho kwa Liverpool kutwaa Kombe.
Liverpool leo watamkosa Mchezaji wao ambae kabla alikuwa Mchezaji na Kipenzi cha Atletico Madrid, Fernando Torres, ambae ameumia goti.
Ingawa Benitez anataka goli la ugenini lakini Meneja wa Atletico Madrid, Quique Sanchez Flores ana maoni kuwa Mshindi atajulikana baada ya mechi ya marudiano huko Anfield wiki ijayo.
Adebayor aonywa kuhusu mechi Jumamosi huko Emirates
Straika wa Manchester City ambae alitokea Arsenal, Emmanuel Adebayor, ameambiwa ni wajibu wake kutumia akili wakati Timu yake Manchester City watakapokuwa Wageni wa Timu yake ya zamani Arsenal Uwanjani Emirates kwenye mechi ya Ligi Kuu Jumamosi hii inayokuja.
Adebayor alikumbana na kashkash ya FA na kupewa onyo kali aliposhangilia goli lake mbele ya Mashabiki wa Arsenal mwezi Septemba Timu hizo zilipocheza mechi ya Ligi na Man City kuifunga Arsenal 4-2 Uwanjani City of Manchester na ushangiliaji huo ulizua hasira toka kwa Mashabiki wa Arsenal.
Mchezaji mwenzake wa Man City ambae pia alitokea Arsenal, Kolo Toure, amemtaka Adebayor apunguze mzuka na alisema kuwa kitendo cha Adebayor katika mechi ya kwanza hakikuwa kizuri.
Mbali ya ushangiliaji wake uliompa onyo la FA, Adebayor pia alifungiwa mechi 3 kwa kitendo chake cha kumtimba Robin van Persie katika mechi hiyo.
Mechi ya Jumamosi ni muhimu mno kwa Man City ambao wako nafasi ya 5 pointi 2 nyuma ya Tottenham walio nafasi ya 4 kwani Timu itakayomaliza nafasi ya 4 inaungana na Timu 3 za juu kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Kwa Arsenal nao kimahesabu bado wanaweza kuwa Mabingwa kwani wako pointi 6 nyuma ya vinara Chelsea huku zimebaki mechi 3.

No comments:

Powered By Blogger