Tuesday 19 August 2008

NIGERIA WAJIKITA FAINALI YA SOKA OLIMPIKI!
Nigeria wamewabamiza Belgium mabao 4-1 na kuingia Fainali ya Soka ya Olimpiki kwa Wanaume na hivyo kujihakikishia angalau Medali ya Fedha ikiwa watashidwa hiyo fainali ambayo watakutana na mshindi kati ya watani wa jadi Brazil au Argentina ambao watapambana katika Nusu Fainali inayoanza muda si mrefu.
Katika Olympic za 1996 huko Atalanta, Marekani Nigeria walitwaa Medali ya Dhahabu baada kushinda Fainali ikiwa na akina Kanu.
Mpaka mapumziko Nigeria ilikuwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na Olubayo Adefemi.
Mchezaji wa Everton Victor Anichebe alitoa pande zuri kwa Chinedu Ogbuke Obasi aliepachika goli la pili, Obasi akafunga la tatu na Chibuzor Okonkwo akapachika la nne.
Laurent Ciman akapata bao la kufuta machozi kwa Belgium ambao bado wana nafasi ya kupata Medali ya Shaba kwani watakutana na timu itakayofungwa kati ya Brazil na Argentina kugombea medali hiyo.

No comments:

Powered By Blogger