Sunday 30 November 2008

KWA MARA NYINGINE TENA DARAJA LA STAMFORD LAVUNJWA!

Chelsea 1 Arsenal 2

Arsenal, timu iliyofutwa kwenye kinyang'anyiro cha LIGI KUU baada ya vipigo mfululizo, leo imezinduka na kuitandika Chelsea wakiwa kwao Stamford Bridge kwa mabao ya Mdachi Robin van Persie.
Johan Djorou wa Arsenal alijifunga mwenyewe baada ya krosi ya Beki wa Chelsea Jose Bosingwa katika dakika ya 31 kumkuta na akashindwa kuifuta.
Lakini katika dakika ya 59, akionekana kuwa ofsaidi, Robin van Persie, alisawazisha na dakika mbili baadae akachomeka bao la ushindi kufuatia kushushiwa na Adebayor kwa kichwa.

MATOKEO MECHI NYINGINE ZA LIGI KUU LEO:

Tottenham 0 Everton 1

Portsmouth 3 Blackburn 2

No comments:

Powered By Blogger