Thursday 4 December 2008

ROY KEANE ANG'OKA SUNDERLAND!

Kukiwa kumebaki siku mbili tu kabla Meneja Roy Keane [37] hajaipeleka timu yake Sunderland Old Trafford kukutana na Bosi wake wa zamani Sir Alex Ferguson wa Manchester United ambako Keane alikuwa Mchezaji na Nahodha mwenye sifa za kipekee, Roy Keane ameamua kuachana na Sunderland.
Roy Keane alianza kazi ya Umeneja Sunderland Agosti 2006 na akaifanya Sunderland iwe Bingwa wa COCA COLA LIGI na kuipandisha LIGI KUU msimu uliofuatia.
Keane aliwanunua Djibril Cisse, Pascal Chimbonda, Anton Ferdinand, El-Hadji Diouf na George McCartney kwa jumla ya Pauni Milioni 30 lakini mbali ya kucheza mechi 15 za LIGI KUU timu hiyo imeshinda mechi 4 tu na wako nafasi ya 18, yaani watatu toka chini!

No comments:

Powered By Blogger