Sunday 30 November 2008

MECHI ZA LIGI KUU JANA:

Aston Villa 0 Fulham 0,

Stoke 1 Hull 1,

Sunderland 1 Bolton 4,

Wigan 2 West Brom 1,

Middlesbrough 0 Newcastle 0

Bolton wamezidi kuwakandamiza Sunderland kwa kuwapa kipigo cha mabao 4-1 nyumbani kwao na kuwafanya wateremke nafasi na kuingia lile kundi la timu 3 za mwisho zilizo nafasi ya kushuka daraja.
Fulham wakicheza nyumbani kwa Aston Villa waligangamara na kulazimisha suluhu ya 0-0.
Wigan, wakiwa nyumbani, walitoka nyuma baada ya kupachikwa bao na timu iliyo mkiani West Brom na kulazimisha ushindi wa 2-1.
Timu zilizopanda daraja msimu huu, Stoke City na Hull City, zilimenyana zenyewe na kujikuta ngoma droo ya 1-1.
Na timu zilizo majirani za Middlesbrough na Newcastle ziliumana vikali lakini hakuna mbabe aliepatikani na mechi ikaisha 0-0.


RATIBA MECHI ZA LEO:

Man City v Man u [saa 10 jioni bongo taimu]

[saa 12 jioni]

Portsmouth v Blackburn

Tottenham v Everton

[saa 1 usiku]

Chelsea v Arsenal

No comments:

Powered By Blogger