Saturday 6 December 2008

EVRA AFUNGIWA MECHI 4 NA FAINI PAUNI 15,000!!!

Beki wa pembeni kushoto wa Mabingwa Manchester United Patrice Evra amefungiwa mechi 4 na kupigwa faini ya Pauni ya 15,000 baada ya FA kumwona ana hatia ya kupigana na Mkata Majani wa Chelsea, Sam Bethell, kosa lililotendeka Stamford Bridge mara tu baada ya mechi ya Man U na Chelsea mnamo tarehe 26 Aprili 2008.
Kufuatia adhabu hii ambayo ataanza kuitumikia Desemba 22 na ambayo Klabu yake Man U wametamka bado wanaitafakari na watajua hivi karibuni nini wafanye, Evra atazikosa mechi za LIGI KUU dhidi ya Stoke, ikifuatiwa na ya Middlesbrough kisha ya Southampton kugombea Kombe la FA na ya mwisho ni mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la CARLING.

Baada ya kifungo hicho, Evra anaweza kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Chelsea kwenye LIGI KUU hapo Januari 11, 2009.
Klabu ya Chelsea nayo imepigwa faini ya Pauni 25,000 kwa kushindwa kumdhibiti mfanyakazi wao Sam Bethell.


SAKATA LA MIDO KUBAGULIWA: Wawili wabambwa na Polisi kutua kortini Jumanne!

Watu wawili wenye umri ya miaka 49 na 23 wanashikiliwa na Polisi kwa kutuhuma za kutoa matusi ya kibaguzi dhidi ya Mchezaji kutoka Misri Mido anaechezea Middlesbrough kwenye mechi dhidi ya Newcastle hapo tarehe 29 Novemba 2008 na watafikishwa Mahakamani Jumanne ijayo.
Mido alilalamika vikali kushambuliwa na Washabiki wa Newcastle kwa misimu miwili mfululizo kibaguzi bila FA kuchukua hatua yeyote.

No comments:

Powered By Blogger