Tuesday 2 December 2008

NDANI YA KABATI LA CRISTIANO RONALDO ZIPO TUZO ZIFUATAZO:

Cristiano Ronaldo, ambae leo alfajiri ameikwaa Tuzo ya Mpira wa Dhahabu[Ballon d'Or] ikimaanisha yeye ndie MCHEZAJI BORA WA ULAYA 2008, tangu atue Manchester United mwaka 2003 ameshatwaa Tuzo kibao.

Mlolongo wa Tuzo hizo, Mwaka aliozichukua na jina lake rasmi kwa Kiingereza ni kama ifuatavyo:

-Mchezaji Bora Chipukizi kwa Wachezaji wa Kulipwa 2004/5 & 2005/6 [FIFPro Special Young Player of the Year]
-Mchezaji Bora Chipukizi kwa Wachezaji wa Kulipwa wa Uingereza 2006/7 [PFA Young Player of the Year]

-Mchezaji Bora Alieteuliwa na Wachezaji wenzake wa Kulipwa Uingereza 2006/7 & 2007/8 [PFA Player's Player of the Year]

-Mchezaji Bora alieteuliwa na Mashabiki 2006/7 & 2007/8 [PFA Fans' Player of the Year]

-Mchezaji Bora alieteuliwa na Waandishi wa Habari wa Soka 2006/7 & 2007/8 [Football Writers' Footballer of the year]

-Mchezaji Bora wa Barclays [Wadhamini wa LIGI KUU] 2006/7 & 2007/8 [Barclays Player of the Season]

-Barclays Buti ya Dhahabu 2007/8 [Barclays Golden Boot]=Mfungaji Bora LIGI KUU

-Buti ya Dhahabu ya Ulaya 2007/8 [European Golden Shoe]=Mfungaji Bora wa Klabu Ulaya

-Fowadi Bora wa UEFA 2007/8 [UEFA Club Forward of the Year]

-Mchezaji Bora wa Klabu za Ulaya 2007/8 [UEFA Club Footballer of the Year]

-Mchezaji Bora wa Wachezaji wa Kulipwa Duniani 2007/8 [FIFPro World Player of the Year]

-Mchezaji Bora wa MEN 2008 [MEN Player of the Year]=MEN ni Gazeti la Manchester Evening News

-Mchezaji Bora wa Manchester United anaevikwa Tuzo ya Sir Matt Busby 2004, 2007 & 2008 [Sir Matt Busby Manchester United Player of the Year]

-Mchezaji Bora wa Manchester United 2007, 2008 [Manchester United Players' Player of the Year]

No comments:

Powered By Blogger