Thursday 4 December 2008

DRO YA NUSU FAINALI YA CARLING CUP KUFANYIKA JUMAMOSI Desemba 6, 2008.

Baada ya Timu za Daraja la chini Burnley na Derby kufuzu kuingia Nusu Fainali hapo juzi baada ya Burnley kuiadhiri Arsenal bao 2-0 na Derby kuwatoa Stoke kwa bao 1-0, jana miamba wa LIGI KUU, Man U ambao ni Mabingwa wa England na Ulaya na Tottenham ambao ni Mabingwa Watetezi wa Kombe hili la CARLING wamefanikiwa nao kuingia Nusu Fainali huku Man U wakiwachakaza Blackburn 5-3 na Tottenham kuwapiga Watford 2-1.

Sasa nani anacheza na nani kwenye Nusu Fainali ya CARLING CUP itajulikana Jumamosi tarehe 6 Desemba 2008 wakati dro maalum itakapofanyika.

Mechi za Nusu Fainali zitatakiwa zichezwe kwa mtindo wa nyumbani na ugenini huku mechi ya kwanza inabidi ichezwe wiki ya kuanzia Januari 5, 2009 na marudiano ni wiki ya kuanzia Januari 19, 2009.

FAINALI itachezwa tarehe 1 Machi 2009.

No comments:

Powered By Blogger