Saturday 6 December 2008

CARLING CUP: NUSU FAINALI= Burnley v Tottenham na Derby v Man United

Dro ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling imefanyika na Timu ya Daraja la chini ya LIGI KUU ambayo mpaka sasa imeshawatoa kwenye muchuano hiyo Timu za vigogo za LIGI KUU za Fulham, Chelsea na Arsenal wamepangiwa kigogo mwingine wa LIGI KUU Tottenham ambao pia ndio Mabingwa Watetezi wa Kombe hilo.
Nao Derby County, timu nyingine ya Daraja la chini ya LIGI KUU, itapambana na Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United.
Nusu Fainali ya Kombe hili zitachezwa kwa mikondo miwili, nyumbani na ugenini, na mechi ya kwanza itachezwa wiki inayoanzia Januari 5, 2009 na marudiano wiki inayoanza Januari 19, 2009.
Fainali itachezwa tarehe 1 Machi 2009.

No comments:

Powered By Blogger