Thursday 4 December 2008

MIDO AILAUMU FA: 'Walifanya msimu uliopita, wamefanya msimu huu hakuna kitakachotokea!!'

Mido, Mchezaji kutoka Misri anaecheza Middlesbrough, amelalamika vikali kushambuliwa na Washabiki wa Newcastle kwa misimu miwili mfululizo kibaguzi bila FA kuchukua hatua.
Mido amesema: 'Waliendelea kuimba ubaguzi, maneno ya kukashifu dini ya Kiislam na bahati mbaya ni Mashabiki haohao wamerudia mara ya pili!'
Akisikitika sana Mido alinung'unika: 'Hii imetokea tena kwa sababu FA haikuchukua hatua mara ya kwanza! Mie sijali nitukanwe binafsi lakini usitukane Uislamu!! Nina hakika hata safari hii hamna lolote litafanyika! Ni ujinga tu!'


KAULI YA MIDO INAFUATIA TAARIFA ZETU TULOTOA MAPEMA [SOMA CHINI]

FA KUCHUNGUZA TUHUMA WASHABIKI WALIMBAGUA MIDO

FA, Chama cha Soka Uingereza, kinachunguza tuhuma kuwa Washabiki wa Newcastle walimkejeli Mido, Mchezaji wa Middlesbrough anaetoka Misri, kibaguzi wakati alipokuwa akipasha moto mwili katika mechi ya ligi kati ya Middlesbrough na Newcastle juzi mechi ambayo iliisha suluhu ya 0-0.Washabiki hao walisikika wakiimba nyimbo za ubaguzi wa rangi wakimlenga Mido.

No comments:

Powered By Blogger