Sunday 30 August 2009

Everton 2 Wigan 1
Ndani ya Uwanja wao Goodison Park, Everton leo wamepata ushindi wao wa kwanza tangu msimu huu uanze walipofunga bao la ushindi kwa penalti dakika za majeruhi baada ya Mshambuliaji Jo kuangushwa ndani ya boksi na Emmerson Boyce wa Wigan na Beki wa pembeni wa kushoto aliewahi kuwa Mchezaji wa Wigan, Leighton Baines, kuifunga penalti hiyo.
Hadi mapumziko mechi hii ilikuwa suluhu 0-0 na kipindi cha pili Paul Scharner wa Wigan aliipatia Wigan bao la kwanza dakika ya 57 lakini Luis Saha akasawazisha dakika ya 62.
Hiki ni kipigo cha 3 mfululizo kwa Wigan baada ya kushinda mechi yao ya ufunguzi ya Ligi Kuu walipowapiga Aston Villa 2-0.
Everton: Howard, Hibbert, Yobo, Distin, Baines, Osman, Neville, Rodwell, Pienaar, Cahill, Saha.
Akiba: Nash, Bilyaletdinov, Jo, Gosling, Fellaini, Duffy, Agard.
Wigan: Pollitt, Melchiot, Boyce, Bramble, Figueroa, N'Zogbia, Thomas, Scharner, Diame, Gomez, Rodallega.
Akiba: Kingson, Edman, Cho, Scotland, Koumas, Sinclair, King.
Refa: Lee Probert (Wiltshire).
Villa 2 Fulham 0
Aston Villa wakicheza kwao Villa Park leo wamewapiga 2-0 Fulham katika mechi ya Ligi Kuu kwa mabao yaliyofungwa na Pantsill aliejifunga mwenyewe dakika 3 tu tangu mchezo uanze kufuatia kona ya Ashley Young na la pili lilipachikwa na Agbonlahor dakika ya 55.
Aston Villa: Friedel, Beye, Cuellar, Clark, Shorey, Petrov, Milner, Sidwell, Reo-Coker, Ashley Young, Agbonlahor.
Akiba: Guzan, Carew, Albrighton, Delph, Heskey, Warnock, Gardner.
Fulham: Schwarzer, Pantsil, Hughes, Hangeland, Konchesky, Dempsey, Kamara, Greening, Etuhu, Duff, Nevland.
Akiba: Zuberbuhler, Kelly, Baird, Gera, Riise, Eddie Johnson, Smalling.
Refa: Steve Bennett (Kent)

No comments:

Powered By Blogger